ASALAMU ALAYKUM.
WAKATI tunaendelea kukusanya michango ya watoto wetu Nairat na
Bisambe ambao wanasumbuliwa na matatizo ya ngozi, Napenda kutoa taarifa
kwamba ahadi ya kwenda hospitali Nairat kulazwa ilikuwa ni tarehe 4 na
kufanyiwa upasuaji ni tarehe 5 mwezi ujao inshallah lakini bahati nzuri
kumetokea shirika la Kimataifa la Sight savers chini ya mradi wake wa
huduma za macho Zanzibar litamdhamini matibabu ya macho Nairat na hivyo
kwa sasa badala ya kusubiri mwezi ujayo matibabu yake yatafanyiwa mwezi
huu inshallah, ambapo leo hii Nairat na Bisambe wanakwenda Dar es Salaam
kwa ajili ya uchunguzi wa macho na hivyo huenda wakalazwa katika
hospitali ya Muhimbili badala ya CCBRT na hilo ni kutokana na
makubaliano kati ya madaktari wa CCBRT na Muhimbili.
Lakini kwanza kwa kuwa Sight saves wanahusika na macho peke yake tena
kwa watoto hivyo basi Nairat ndio atakayenufaika na huduma hii ambayo
baada ya kufanyiwa vipimo na kukamilika taratibu zote basi atalazwa hapo
Muhimbili na kuendelea na hatua zinazofuata za matibabu. Tumuombee dua
inshallah afanikiwe na kila kitu kiwe chepesi kwa uwezo wake Jalali Mola
wa uulimwengu wote.
Na baada ya hapo tukishajua suala la macho sasa tutaendelea katika
suala la ngozi na katika hilo watalazimika kufanyiwa vipimo wote wawili
na tukishajua kitachoendelea tunaendelea kuarifiana lakini kwa sasa
tunamshughulikia Nairat ambaye yeye anahitajika matibabu ya haraka
kuhusiana na macho yake ambayo yameathirika na kuonekana kuwa ana kensa.
Mwenyeenzi Mungu ndio Mjuzi na ndiye mweye uwezo wa kulifanya gumu kuwa
jepesi hivyo dua kwa watoto hawa ni muhimu sana kwetu inshallah.
Hadi tulipofikia hapa katika kushughulikia masuala la watoto hawa
tunakwenda vizuri Alhamdulillah na mambo yote takriban yanakwenda kwa
utaratibu mzuri na kwa wepesi kabisa tunamuomba Mwenyeenzi Mungu atupe
nguvu ya kuendelea kushugulikia suala hili hadi kufikia kikomo.
Kwa ufupi kabisa katika suala la hali ya Bisambe ambaye yeye ni mdomo
wake ndio wenye kuwa na vidonda na kukatikakatika bado tatizo lake
anaendelea nalo licha ya kuchukuliwa vipimo na kutumia dawa kadhaa
lakini hajapata unafuu sana ila angalau kidogo hali yake sio kama awali
kwa kuwa angalau anaweza kula vizuri kwa sasa ingawa sio nyakati zote
hutegemea na yale maumivu anayopata.
Kwa upande wa Nairat vidonda ndani ya macho vimepona, vidonda kwenye
pua ndani na nje pia vimekauka ila vidonda katika mdomo bado vinamsumbua
ingawa kwa kiasi kikubwa vinaonekana kukauka na kujirudia tena lakini
ile kutoka damu tokea nilipomchukua nyumbani kwangu wili ya pili sasa
sijaona hata siku moja kutoka damu na ulimi wake sasa naona upo safi
vidonda vimekauka na angalau anakula vizuri, na ule mwili wake tokea
kuanza kumpaka dawa na kutomruhusu kutoka nje amebadilika na sasa baada
ya kufuata masharti ya kutokaa juani ameanza kubadilika rangi ule weusi
yaani madodoa meusi katika mwili wake yameanza kufifia na nadhani
akiendelea zaidi inshallah yatakwisha ingawa itachelewa lakini naamini
atabadilika kwa uwezo wake Allah.
Kuhusiana na fedha tulizopokea hadi sasa tumeanza kuzitumia kwa
vipimo mbali mbali tokea walipoanza vipimo vya hapa hapa nyumbani Al
Rahma, Mnazi Mmoja na hatimae huko CCBRT na leo huko Muhimbili na pia
tumenunua dawa na vifaa ambavyo Nairat ametakiwa kuwa navyo kwa ajili ya
kujikinga na jua pamoja na dawa maalumu ambazo anatakiwa atumie muda
wote na hivyo risiti zote zipo yaani nakusuadia kwamba hakuna fedha
ambayo inatumika au itatumika bila ya maelezo na wala hakuna fedha
iliyotoka bila ya utaratibu wa matibabu. Mama Nairat yaani Bi Khadija
Mohammed amekubali kutochukua fedha kwa kuogopea kuja kuzitumia kwa
shughuli nyengine nje ya lengo yaani ‘matibabu ya watoto’ na hivyo
ameniachia mimi kwa ridhaa yake niwe nashughulikia masuala yote hayo.
Nami kwa kuwa ameniamini naahidi kwenu nyote mliotoea fedha zenu kwamba
fedha hizo zitatumika kwa malengo yaliokusudiwa na inshallah maana
lazima tuweke msisitizo wa kumtangulia ALLAH mbele katika suala la fedha
kwamba nitajitahidi malengo tuliokusudiwa yafikiwe.
Kwa niaba yangu binafsi na mama mzazi wa Nairat Bi Khadija Mohammed
tunawashukuru wote wale ambao wamekuwa karibu sana nasi katika jambo
hili kwa kutoa michango yao mbali mbali, kifedha, usafiri, huduma na
hata mawazo na kutupa fikra za kufanya katika kufikia lengo la tiba
tokea tulipoanza mbio za kutafuta ufumbuzi wa matatizo ya watoto hawa.
Kwa kila hatua tutaelezana inshaalla